TAARIFA YA AWALI KUINGUA SOKO L SIDO
Natoa pole kwa wote walioathirika na janga la moto kwa wafanyabiashara
soko la Sido. Soko la sido lilianza kuungua saa 21.32 Hrs jana usiku na
kuteketeza mali za wafanyabiashara wa soko la sido
Pamoja na kutoa
pole niwashukuru wananchi, vyombo vya ulinzi kwa ushirikiano na kazi
kubwa YA kudhibiti moto usiendelee kuleta madhara makubwa zaidi
Serikali kupitia Mkuu wa wilaya ya Mbeya imeunda kamati ya kufanya tathmini ya kujua hasara na chanzo cha Moto huo
Tunaomba wananchi waendelee kuwa watulivu na watoe ushirikiano kwa kamati hiyo ili tuweze kujua chanzo cha moto na hasara iliyopatikana
Tunaomba wananchi waendelee kuwa watulivu na watoe ushirikiano kwa kamati hiyo ili tuweze kujua chanzo cha moto na hasara iliyopatikana
Aidha vyombo vya ulinzi vinaendelea kuchunguza kujua kama moto huo
utakuwa umesababishwa na mtu/ watu uchunguzi huo bado unaendelea. Nirudie tena kuwapa pole wote walioathirika na janga na mungu awatie nguvu ktk kipindi hiki Kigumu
Amos G.Makalla


0 comments:
Post a Comment