Monday, August 21, 2017

Image may contain: 1 person, outdoor
KIFO CHA MTEMI Mbula Mtelya Kasanda maarufu MTEMI MILAMBO!

SIMULIZI za Padre Simeon Lourdel JUU YA KIFO CHA MTEMI MILAMBO. Father Lourdel aliishi UNYAMWEZINI tangu tarehe 5 februari 1871.
ukweli ni upi?


VITA KATI KAPELA NA MIRAMBO.
Mtemi Ndwikwa Kapela II, amesimulia kuwa : Kapela alikuwa na tabia ya kutambikia kwanza kabla ya kuanza vita, wakati anajiandaa kupigana na Mirambo alifanya hivyo hivyo
Aliwaalika « Waswezi », viongozi wa kuomba mizimu. Aliwaalika na wakaenda kwa Kapela na kuingia katika kijumba cha matambiko (kagondo) wakakaa humo usiku kucha wakiwa pamoja na Kapela mwenyewe. Kulipopambazuka aliwapeleka kwenye mti uliopandwa juu ya kaburi la watoto wake ambao walikuwa mapacha, (Kulwa na Doto).
 

MTEMI MIRAMBO AFANYA MATAMBIKO KABLA VITA.
Padre Simeon Lourdel wa Shirika la Mapadre Weupe (White Fathers) ambae wakati huo alikuwa rafiki yake Mirambo, katika kitabu chake kinachosimulia kuwa « askari wa Mirambo wakati wanacheza ngoma ya ibada ya matambiko walikuwa wamevaa manyoya ya mbuzi mabegani, walikuwa wakiimba « Kapela ufililie mbali, Kapela ufifilie mbali… » Walirudia rudia maneno hayo. Mirambo alipomuaga mama yake mdogo Masele kwamba anajiandaa kwenda kupigana na Kapela. Mama yake akamshauri kwamba « mwanangu usiende kupigana na Kapela kwa kuwa ni mjomba wako na huko ndiko nyumbani kwetu »..
Mirambo akamjibu « mama acha, kama unamtetea nenda kujiunga na wachawi wenzako akina Subi » (Subi alikuwa ni dada yake na Kapela pamoja na mama yake Mirambo – Nyakasi, na Masele mdogo wao) Baada ya matambiko, Mtemi Mirambo na askari wake waliondoka kwenda vitani, wakafika katika kambi yao ya huko Manguwa.

MTEMI KAPELA AFANYA MATAMBIKO KABLA VITA..
Mtemi Ndwikwa Kapela II, amesimulia kuwa : Kapela alikuwa na tabia ya kutambikia kwanza kabla ya kuanza vita, wakati anajiandaa kupigana na Mirambo alifanya hivyo hivyo
Aliwaalika « Waswezi », viongozi wa kuomba mizimu. Aliwaalika na wakaenda kwa Kapela na kuingia katika kijumba cha matambiko (kagondo) wakakaa humo usiku kucha wakiwa pamoja na Kapela mwenyewe. Kulipopambazuka aliwapeleka kwenye mti uliopandwa juu ya kaburi la watoto wake ambao walikuwa mapacha, (Kulwa na Doto).
19
Waszezi wakazunguka mti huo huku wamevaa mavazi yao ya kutambikia kichawani (kishingo). Pia askari walileta silaha zao na kuzisimika chini ya mti huo. Kisha kiongozi na waswezi aliwapulizia maji yaliyochanganywa na mtama (kafupa) kuwaombea dua la ushindi.
Mtemi Kapela wakati wa maandalizi yake ya vita alikwenda Kigoma na kupata pembe pamoja na mkuki alivyovitumia vikiwa na dawa. Pembe hilo alilitumia kuonyesha ishara ya hatari. Aliliweka katika mlango wa ikulu (Luzonzo), wakati wa hatari lilikuwa likivuja damu na akilikuta linatoka maji alijua kuwa hakuna hatari yoyote. Waswezi walitunga wimbo kulisifu pembe hilo wakiimba : « Nalini pembe lyane nalifunya kule ma Bhuha ulu wahaya kubuma ng’wafurani na kuloga lusalo » wimbo huo ulifahamisha sana kwa Wanyamwezi hadI leo hii.... Mkuki na aliutumia alipokuwa akitembelea maeneo ya vita - ulikuwa umefungiwa hirizi katika ncha za makali yake, akikutana na adui yake ana kwa ana aliuelekea makali yake kwa adui na huyo alikufa pale pale.

VITA
 

Mtemi Ndwikwa Kapela II husimulia kuwa vita vilianza mwezi octoba mwaka 1883, na vilidumu kwa mwaka mzima. Mtemi Mirambo alikuwa amechimba handaki lililoanzia kijiji cha Manguwa, huko Igalula ambako ndiko kulikuwa na kambi ya Mirambo. Tarehe 1/2/1883 majeshi ya Mirambo yakitokea upande wa kaskazini yalikaribia ikulu ya Kapela . Kapela alipoona kuwa karibu Ikulu yake itatekwa, akatumia mbinu na kuwaambia askari wake kuwa wapige kelele wakisema « ndugu, tuache vita » Majeshi ya Mirambo yakaamini kweli mjomba wake anaomba waache vita kwa kujali undugu. Kulikuwepo jemadari wa Kapela, mtoto wa Subi alipoona mbinu hizi zinafanikiwa, waliwasongelea askari wa Mirambo na kuanza kuwashambulia kwa bunduki. Kulikuwepo jemadari wa Kapela, mtoto wa Subi alipoona mbinu hizi zinafanikiwa, waliwasongelea askari wa Mirambo na kuanza kuwashambulia kwa bunduki. Mtoto huyu wa Subi aitwaye Fuzigwalyuba, ndiye alyeanza kufyatua risasi, na baadaye askari wa Mirambo wakabana na kumpiga risasi na kufa. Kapela aliposikia kwamba mtoto wake amekufa, akalia na kusema « Namala bhanhu » yaani nimemaliza watu.
Dada yake Subi akawaambia kuwa, « kumbe wewe (KAPELA) bado ni mtoto, nyamaza, tutakapoipata maiti yake, tutakuwa tumeshinda ». Basi majeshi ya Kapela yakafanya juu chini yakafaulu kuipata ile maiti na kuipeleka ikulu. Palipokuwepo na wazee wanawake ambao Kapela aliwatumia kama wachawi wake wakati wa vita, nao ni :
 

Ngoboizizi, Wadumwa, Kabula Shingona. Wazee hawa walikuwa wanaambatana na Subi kwa kazi zao za kichawi. Subi alichukua tunda la mti uitwao mwicha – akalipakata kama mtoto na kumbembeleza na kusema « nyamaza Mirambo », wale wazee wengine wakawa wanapiga vigelegele, wakichukua pia dawa ambayo iliwafanya wasionekana mpaka kwenye shimo ambalo alikuwa akilitumia Mirambo kwa mapumziko. Wakamkuta humo ndani na kumchukua kichawi na kumpeleka kwa Kapela....

Walipomfikisha kwa Kapela, akachinjwa mbwa mweusi na nyama yake ikachanganywa na sehemu kidogo ya Fuzigwalyuba na kutayarishwa kitoweo. Wakati maandalizi yanafanywa ya chakula hicho, Mirambo alikuwa kikalishwa kwenye kiti pamoja na Kapela mjomba wake akiwa hajifahamu, Chakula kilipokuwa tayari alipelekewa Mirambo ; na kuanza kula, mara akapata fahamu na kumuona Kapela ana kwa ana, ndipo Subi akamwambia Mirambo « kula tu mwanangu, hapa upo nyumbani kwa wazazi wako ». Subi akamwuliza Kapela « je una lolote la kumwuliza huyu ndiye mpwao » Kapela akamwuliza Mirambo « Mpwa wangu umeamua kweli kupigana vita na mimi mjombao ? » Mirambo hakujibu neno. Na Mirambo hakupata tena akili akawa amepotewa na fahamu. Subi akamuliza Kapela kaka yake « vipi utamfanya nini mpwao ? »
Kapela akasema « ni lazima nimuue ». Akaagiza afungwe kamba shingoni - wale wazee « wa kike » (wanawake) wakasaidiana kuvuta ile kamba na kuifunga juu katika boriti ya nyumba. Subi akachukua « ki-chungu » kidogo knaitwa « shindye » na kukinga mkojo wa Mirambo na kumpa Kapela anywe kidogo. Baadaye mwili wa Mirambo ukashushwa chini na... kichwa chake kikanyolewa nywele. hizo nywele na mkojo vipo hadi leo hii. Huo ndio ukawa mwishao wa Mirambo!


Baada ya Mirambo kufa, Subi pamoja na wale wazee wawili wakaibeba maiti bila kuonekana na kuirudisha katika handaki lake, katika sehemu inayoitwa Kundikili. Wakamlaza na kuonekana akiwa amelala. Inasemekana kwamba kifo cha Mirambo kilikuwa cha kunyongwa tarehe 2/12/1884, siku ya alhamisi. Mirambo akiwa amelazwa katika handaki lake si hai tena, majeshi yake hayakufahamu bado kama amekufa ; kesho yake asubuhi yalijiandaa kwa mashambulizi kuelekea ikulu ya Kapela. Baada ya kuona kuwa Mirambo anachelewa kutoka, hapo ndipo mdogo wake na Mirambo aitwaye Mpanda Chalo akatumwa na Ntinginya ili akamwambie Mirambo waanze mashambulizi. Mpanda Chalo alipoingia katika handaki akakuta Mirambo kisha kufa. Akapeleka habari kwa Mtemi Ntinginya kuwa Mirambo ameshakufa. Basi hapo Mtemi Ntinginya akasema kuwa sasa hakuna haja ya kuendelea na vita - Mungu kishaamua. Mpanda Chalo asema kuwa : “ kwa kuwa mimi nipo vita vitaendelea tu”. Ntinginya akasema :“ sisi tulikuwa na mkataba na Mirambo wa kumsaidia lakini sio wewe, hatukujui !”

MWISHO WA VITA VYA MIRAMBO NA KAPELA.
Mara tu baada ya kifo cha Mirambo, Watemi wote waliokuja kumsaidia Mirambo walikusanya majeshi yao yote na kuyaamuru kurudi nyumbani. Wakati huo Mapadre wa Shirika la Mapadre Weupe ambao walikuwa marafiki wa Mtemi Mirambo wakiongozwa na Padre Simeon Lourdel, walifika kumletea dawa Mirambo ya ugonjwa wa madonda ya koo. Habari za kuaminika zinasema kuwa Mirambo alikuwa na magonjwa mengi. Padre Lourdel aliunga mkono maelezo ya Mtemi Ntinginya wa Usongo ya kusisitisha mapigano.


...Wakateuliwa watu wa kubeba maiti ya Mirambo na kuirudisha Ulyankulu, katika ikulu yake ya Ikonongo, kupitia Ngokolo (Iwe lya shinga), wakaongozana pamoja na Padre. Walipofika Iwe Lya Shinga, mama yake (mdogo) aliipokea maiti, kisha Padre akafanya ibada ya marehemu.Baadaye maiti ikapelekwa Ushetu katika ikulu ya Mtemi Magope, iitwayo Itulamashiki. Magope akaiosha maiti ile kuonyesha uhusiano waliokuwa nao kati yake na Mirambo. Mara baada ya tukio hilo safari iliendelea hadi Ulyankulu katika ikulu ya Mirambo, Ikonongo. Mrithi wa Mirambo alikuwa mdogo wake Mpandachalo.
UTATA...
 

Kifo cha Mirambo katika maelezo haya kinataufautiana na maelezo yaliyomo katika kitabu kilichoandikwa na Padre John Kabeya. Maelezo yaliomo katika kitabu cha Kabeya yanamwelezea Mtemi Mirambo, lakini katika maelezo haya ya Padre Simeon Lourdel ni maelezo hasa ya Mtemi Kapela na maisha yake. Hivyo basi haya yote yamepatikana huenda kwa sababu ya kumsifia Mtemi Kapela na yale ya Kabeya ilikuwa kumsifia Mtemi Mirambo. 

Kila upande unasimulia sifa na ushujaa wa Mtemi anayehusika. Ni jambo la kutia moyo na kutoa nafasi ya uchunguzi zaidi kwa wataalamu wa fani ya mambo ya kihistoria na ya kale kutafuta maelezo sahihi ya KIFO CHA MTEMI MILAMBO

0 comments:

Post a Comment