Monday, September 4, 2017

Image result for Neymar and Mbappe at PSG

Klabu ya Paris Saint-Germain ndiyo timu pekee iliyotumia fedha nyingi kusajili duniani baada ya kutua kwa Kylian Mbappe kutoka Monaco kunafanya kikosi chao cha kwanza XI kuwa cha thamani ya euro 640milioni.

Zaidi ya euro 418milioni zimetumika kuwanunua wachezaji wanne tu msimu huu 2017 (Yuri Berchiche, Dani Alves, Neymar na Mbappe), Les Parisiens imeusambaratisha utaji wa Russia uliotumia kununua nyota wa Monaco katika miaka ya karibuni.
Neymar alinunulia wa euro 222milioni kutoka Barcelona uhamisha uliotikisa dunia kutokana na dau hilo kubwa.
PSG imepiga bao lingine kwa kumnyakuwa Mbappe kwa mkopo wa muda mrefu na wanategemea kulipa euro 180milioni msimu ujao na kumchukua moja kwa moja.
Ni kipa pekee Alphonse Areola na Adrien Rabiot waliopatikana kupitia akademi ya miamba hiyo ya Ligue 1 huku Alves akiwasiri kutoka Juventus akiwa mchezaji huru.
Pamoja na mabeki wengine Thiago Silva na Marquinhos, wote walinunua kutoka ligi ya Italia ‘Serie A’ kwa euro 42milioni na euro 31.5milioni, huku beki wa kushoto Layvin Kurzawa akichukuliwa kwa euro 25milioni.
Marco Verratti alinunuliwa euro 12 milioni kutoka Pescara huku Angel Di Maria akiwaghalimu euro 63milioni kutoka Manchester United.
  1. Areola: Academy (2012)
  2. Dani Alves: Huru (Juventus, 2017)
  3. Thiago Silva: euros 42m (Milan, 2012)
  4. Marquinhos: euros 31.5m (Roma, 2013)
  5. Kurzawa: euros 25m (Monaco, 2015)
  6. Verratti: euros 12m (Pescara, 2012)
  7. Di María: euros 63m (United, 2015)
  8. Rabiot: Academy (2012)
  9. Neymar: euros 222m (Barcelona, 2017)
  10. 10.Cavani: euros 64.5m (Napoli, 2013)
  11. Mbappe: euros 180m italipwa msimu ujao (Monaco, 2017)
Categories:

0 comments:

Post a Comment