Wednesday, September 6, 2017

Image result for dele alli middle fingerKiungo wa kati wa Uingereza , Dele Alli amesema ishara aliyoitumia ya kidole cha kati wakati wa michuano ya kufuzu kwa Kombe la dunia dhidi ya Slovakia ilimlenga mchezaji mwenzake.
Picha zilizoonyeshwa kwenye runinga zilimuonyesha Alli akiomyesha ishara hiyo dakika ya 77 siku ya Jumatatu walipopata ushindi wa 2-1 katika uwanja wa Wembley.

Dele Alli alifunguka kupitia ukurasa wake wa Twitter - ''Kuyaweka bayana, ishara hiyo ilikuwa ni ya utani kati yangu na rafiki yangu Kyle Walker,''  ''Naomba msamaa kwa kosa lolote lililotendeka.''

Shirikisho la kandanda duniani (Fifa) linasubiri ripoti kutoka kwa viongozi wa mechi hiyo, inayotarajiwa kutolewa mwishoni mwa wiki, kabla ya kutoa maamuzi iwapo kumfungulia mchezaji mashtaka kwa ukosefu wa nidhamu au la.

Hapo awali ilionekama ishara hiyo iliyofanywa na Alli kwa Turpin ambaye alioneka wakibadilishana maneno alipokuwa akitolewa uwanjani katika dakika 93 ya mchezo. Alli na beki Walker walikuwa wakiichezea klabu ya Spurs hadi pale Walker alipojiunga na Manchester City majira ya joto.


Meneja wa Uingereza Gareth Southgate amesema wawili hao , walikuwa ''wanachokozana,'' aliongeza '' wako na njia za kushangaza kama njia ya mawasiliano yao.''
Hasira ya Alli hapo awali ilizuwa wasiwasi.

Alikosa mechi ya kuwania taji la ligi ya Premia 2015-16 baada ya kumpiga kofi mchezaji wa Bromwich Albion, Claudio Yacob, na alitolewa uwanjani kwa kufanya kosa jingine dhidi ya kiungo wa Gent Brecht Dejaegere wakati wa mechi ya ligi ya bara ulaya mwezi Febrauri iliyopita. 


Uingereza ilianza mechi yao vibaya siku ya Jumatatu , kupitia bao la Stanislav Lobotka alilolifunga katika dakika tatu ya mchezo. Eric Dier alisawazisha baada ya mpira kupigwa kutoka kwa kona, kabla Marcus Rashford kufunga na kuiongozea makali timu yake.

Uingereza wako kileleni na alama tano, mbele ya Slovakia katika kundi F wakiwa bado wamesalia na michezo miwili. Mshindi katika makundi atafuzu moja kwa moja kwa kombe la dunia msimu ujao litakaloandaliwa huko Urusi, huku watakao kuwa katika nafasi ya pili wakicheza mechi za marudiano.
Categories:

0 comments:

Post a Comment