Simba
na Azam zitakutana katika mchezo wa Ligi Kuu Jumamosi hii kwenye Uwanja
wa Uhuru, huku Simba ikiwa na kumbukumbu ya kufungwa kwenye mchezo wa
mwisho uliozikutanisha timu hizo.


Mo Ibrahim alisema kwa sasa kikosi cha Simba kina njaa ya mafanikio na itakuwa vigumu kuziacha pointi tatu watakapokutana na Azam.
“Tuna
timu nzuri iliyokamilika, kukosa mabao ni sehemu ya mpira. Tunakwenda
kujirekebisha kabla ya kucheza na Azam,”alisema Mo ambaye alifunga bao
pekee katika mechi ya nusu fainali ya Kombe la Fa iliyozikutanisha timu
hizo, Mei mwaka huu.
Jumapili iliyopita, Simba ilicheza
mechi ya kirafiki dhidi ya Hardrock ya Pemba na licha ya kuibuka na
ushindi wa mabao 5-0 washambuluaji Laudit Mavugo na Juma Liuzio walikosa
mabao mengi ya wazi.
Kocha Msaidizi wa Simba, Jackson
Mayanja alisema Simba itafanya vizuri kwenye mchezo wa Azam kwakuwa
baadhi ya wachezaji wake muhimu watakuwa wamerudi kikosini.
“Wanasimba
wawe watulivu, kila mchezaji aliyesajiliwa ana nafasi yake. Niyonzima,
Okwi na Juuko tumewakosa leo, lakini ni wachezaji muhimu. Kujiandaa
kwetu ni kuhakikisha tunashinda kila mchezo,”alisema Mayanja, akiwatetea
washambuliaji wake.
0 comments:
Post a Comment