Tuesday, September 5, 2017

IMG_0760.JPG
IMG_0761.JPG Waziri Mkuu wa zamani na Mgombea urais kwa tiketi ya UKAWA mwaka 2015, Edward Ngoyai Lowassa, kama ilivyo kwa wafuasi wengi wa CHADEMA, wamejikuta katika mtego mgumu kuutegua tangu Mahakama Kuu nchini Kenya kutengua ushindi wa Rais Mteule Uhuru Kenyatta na kuamuru kurudiwa kwa uchaguzi ndani ya siku 60.

Mara baada ya Uhuru kupokwa ushindi, Lowassa alifanya mahojiano na Azam Tv na kuahidi kwenda tena nchini Kenya kumpigia kampeni Uhuru, endapo angemuhita.

Hata hivyo wikiendi hii alifanya tena mahojiano na Gazeti la Jamhuri na kudai kuwa, Mahakama Kuu ya Kenya imetoa haki kwa watu (NASA) waliokuwa njiani kuporwa haki yao.

Kwa Hali hiyo, Lowassa na CHADEMA wanajua fika kwamba Uhuru alikuwa amepoka haki ya Odinga. Sasa Lowassa kwa nini anataka tena kumpigia kampeni mtu aliyeiba kura, huku wao ndio huwa wanalalamika kuwa, kura zao ziliibwa mwaka 2015.

Ni aibu kuwa, wafuasi na vyombo vya habari vinavyotetea wapinzani, wamekomalia kusifia sijui Uhuru wa Mahakama nchini Kenya na kusahau issue muhimu "wizi wa kura."

Wapinzani wameanza kumtupa mkono kidogokidogo baada ya Uhuru kutishia kuwashughulikia majaji waliotoa maamuzi hayo. Dah!! hata ndiyo ya "Mgema akisifiwa, tembo hutia maji;" na "Aisifuye mvua imemnyea."

0 comments:

Post a Comment