
Kocha Mkuu wa mabingwa watetezi Ligi Kuu Tanzania bara Yanga Sc, George Lwandamina, ametua tangu usiku wa kuamkia jana
akitokea kwenye msiba wa baba yake.
Lwandamina amethibitisha
ameomba kutafutiwa mtaalamu wa matibabu ya viungo atakayesaidiana na
daktari wa timu hiyo Dk. Edward Bavu.
Mmoja wa viongozi wa Yanga alisema tayari maombi hayo ambayo hata wao wameyakubali, yameshaanza kufanyiwa kazi kwa kumtafuta mtaalamu huyo kwa kuangalia ndani na nje ya nchi atakayefanya kazi hiyo.
Lwandamina alisema: “Nikweli nimewaomba wanitafutie huyo mtu, sawa sasa tuna daktari wa timu lakini tunatakiwa sasa kufikiria mbali zaidi kumaliza hali kama hii ya kuwa na wachezaji wengi muhimu majeruhi kama hivi na hili linaweza kuwa tatizo zaidi unapokuwa katika mashindano makubwa ya Afrika ambayo hayana muda wa kupoteza kila mchezo ni muhimu.”
0 comments:
Post a Comment