Kumekua na tatizo la upungufu wa maziwa kwa wanawake wanao nyonyesha hivyo ziko njia ambazo zinaweza kuongeza uzalishaji wa maziwa.
Mama anae nyonyesha anaweza kupika Uji wa pilipili manga amabo ni mwepesi na kunywa mara 2 kwa siku ambapo ni asubuhi na jioni.
Njia ingine ni mbegu za maboga, Mama anae nyonyesha anaweza kuzitafuna au kuchanganya kwenye uji na hata chai ambapo anaweza kunywa mara mbili kwa kwa siku.
Hata hivyo anaweza kutengeneza Juice ya karoti na kchanganya na tangawizi kisha kunywa mara 2 kwa siku
Aidha Tende pia ni njia nzuri kwa kutafuna vipande vi 3 -4 kwa siku au kutoa mbegu ndani ya tende na kusaga kwenye blenda kisha kuchanganya na maziwa fresh na kunywa mara 2 kwa siku.
Lakini pia Supu ya samaki au nyama iliyo changanywa na mboga mboga inaweza kusaidia ikiwa pamoja na Maji ya kunywa ni muhimu zaidi kunywa kwa wingi.

0 comments:
Post a Comment