Shirikisho la soka la Ivory Coast limesema kuwa huenda likasusia mechi
ya kufuzu kwa dimba la mabingwa barani Afrika dhidi ya wapinzani wao
Sierra Leone ikihofia kuenea kwa Ebola
Ivory Coast kususia mechi na Sierra Leone ikihofia kuenea kwa Ebola
Mchuano huo ambao umeratibiwa kuchezwa mjini Abidjan tarehe 6 Septemba
umeibua taharuki miongoni mwa maafisa wa Afya na serikali kuu inatishia
kuipiga marufuku
Hofu hiyo inatokana na kuenea kwa homa ya Ebola katikamataifa 5 kanda ya Afrika Magharibi ikiwemo Sierra
Ivory Coast kususia mechi na Sierra Leone ikihofia kuenea kwa Ebola
"Kwa mujibu wa msemaji wa shirikisho la soka la
Ivory Coast Malick Tohe, ikiwa wataruhusiwa kuihamisha mechi hiyo hadi
taifa la tatu iwapo CAF itaruhusu.
Tayari Sierra Leone imetaja kikosi cha
wachezaji wanaocheza nje ya Sierra Leone ilikuepusha hatari ya kueneza
Ebola Ivory Coast .
Sierra Leone imeagiza maafisa wote wa ukufunzi kufanyiwa uchunguzi wa kutosha kabla ya kuingia Ivory Coast .
Ivory Coast kususia mechi na Sierra Leone ikihofia kuenea kwa Ebola
Shirikisho la soka barani Afrika limekataa
katakata kubadilisha kutakapoandaliwa mechi za kufuzu licha ya hatari
ya maambukizi .
Hadi kufikia sasa haijulikani iwapo CAF
itaichukulia hatua zaidi Ivory Coast iwapo itasusia kuchuana na Sierra
Leone au itaruhusiwa kuendelea na mechi za kufuzu
0 comments:
Post a Comment