Raia mmoja wa Uingereza anayeishi nchini Sierra leone ameambukizwa virusi vya ugonjwa wa Ebola
Idara ya afya imethibitisha kisa hicho
Tangu mwezi machi zaidi ya watu 1400 wameripotiwa kufariki magharibi mwa Afrika
dara ya afya imesema kuwa raia wa kwanza mwingereza kuambukizwa ugonjwa huo alikuwa anaishi Sierra Leone
Taifa hilo ni miongoni mwa mataifa ambayo yameathiriwa vibaya na ugonjwa huo
Iwapo atapewa matibabu nchini Uingereza mgonjwa huyo ana uwezekano
mkubwa wa kupata nafuu kwa sababu hospitali za Sierra Leone zimejaa
waathiriwa wa ugonjwa huo hatari ambao unaendelea kuenea kwa kasi.
Eneo la kuwatenga wagonjwa tayari limebuniwa katika hospitali ya Royal free mjini London.
Kufikia sasa hakuna tiba ya ugonjwa wa
ebola,ijapokuwa dawa ya majaribio iliwasaidia raia wawili wa Marekani
kupona huku maafisa watatu wa afya pia wakionyesha dalili za kupata
nafuu walipoitumia dawa hiyo nchini Liberia.
Katika mataifa ya afrika magharibi wakaazi wengi
wamekuwa wakiogopa kuwatoa ndugu zao wanaoathiriwa na ebola kwa hofu ya
kutowaona tena
0 comments:
Post a Comment