Saturday, September 6, 2014

 


Kituo  cha polisi kilichopo ushirombo wilayani Bukombe  mkoani Geita  kimevamiwa  na majambazi usiku wa saa tisa kuamkia leo  huku  askari wawili wakiuawa na watatu wakijeruhiwa  vibaya



Ambapo taarifa za awali  zinasema kuwa licha ya matukio hayo  wamelipua  chumba cha kuwekea silaha  na zingine kuondoka nazo,pia wamefanikiwa kuondoka na  bunduki zaidi ya 5  aina ya SMG na kutokomea nazo.



Watu wamekusanyika  kituoni hapo  kushuhudia huku kituo hicho  kikiwa kimezungushiwa  kamba nyekundu kwa kusitisha huduma  na mahabusu  waliokuwemo wamehamishwa.



Hata hivyo kamanda wa jeshi la polisi  mkoani Geita Joseph Konyo yupo katika eneo la tukio kwa uchunguzi zaidi.


Tutawaletea taarifa kamili hivi punde, endelea kutembeleafarajimfinanga.com

0 comments:

Post a Comment