Monday, September 22, 2014

RB namba WH/RB/6335/2014-SHAMBULIO LA KUDHURU MWILI kwenye Kituo cha Polisi cha Wazo Hill, Tegeta jijini Dar, imemtia mbaroni mtangazaji maarufu Bongo aitwaye Hanifa Hamidu ‘Lady Hanifa’ na mwenzake aliyetajwa kwa jina moja la Aneth kwa madai ya kutaka kumuua mhudumu wa baa aliyetambulika kwa jina la Aika Andrew (32).

Mtangazaji maarufu Bongo aitwaye Hanifa Hamidu anayetuhumiwa kumshambuli mhudumu wa baa.
Uchunguzi wa gazeti hili ulibaini kwamba sakata hilo la kusikitisha lilijiri wiki iliyopita kwenye baa maarufu ya Shayo iliyopo Tegeta, Dar.

0 comments:

Post a Comment