MBUNGE
wa Jimbo la Urambo Mashariki Samwel Sitta, amepokelewa kwa kishindo
Jimboni kwake Urambo na kuhutubia katika Viwanja vya Mwananchi Square.
Sitta
akihutubia wapigakura wake alielezea jinsi mchakato wa Bunge Maalum la
Katiba ulivyokwenda hadi alipokabidhi Katiba inayopendekezwa kwa Rais
Dkt.Jakaya Kikwete.
Katika
hotuba yake hiyo, Sitta ambaye alikuwa Mwenyekiti wa bunge hilo,
alielezea jinsi katiba ilivyotoa haki za wakulima, wafugaji, haki za
watoto, baraza la vijana la Taifa, hamsini kwa hamsini kwa wanawake
katika nafasi za uongozi na mengineyo.
Aidha,
amewataka wana Urambo na watanzania kuipitia Katiba inayopendekezwa kwa
kina na ufasaha kwani imekidhi vigezo na matakwa ya wananchi yenye
maslahi mapana ya vizazi kwa vizazi.


0 comments:
Post a Comment