Vijana wa CHADEMA wamepoteza matumaini na chama chao na Viongozi wao
Mwaka huu
wa 2015, ni mwaka wa uchaguzi mkuu, ni mwaka ambao kama taifa
tunatagemea kupata amir jeshi mkuu mpya na rais wa awamu ya tano wa
jamhuri yetu. Vyama mbalimbali vya siasa vinapambana na kujiandaa
kuhakikisha kuwa amir jeshi huyo anatokana na wao. CCM kama chama tawala
kinajiandaa kwa hili na upo mnyukano mkubwa ndani ya chama wa
kuhakikisha kuwa anapatikana Rais Bora na Mwenyekiti muadilifu wa Chama
hicho.
Vijana katika sehemu zote,
katika taasisi hizi za kisiasa wamekuwa ndio wachakalikaji wakubwa, ndio
wapiga debe wa wagombea mbalimbali ambao wamekwishatangaza nia na wale
ambao bado nia yao haijawekwa wazi. Kwenye Mitandao ya kijamii, katika
magazeti, wordpress na kwingineko vijana wanachuana kuwapamba wagombea
wao.
Vijana ndani ya Chama cha
mapinduzi wamekuwa katika vita baina yao inayotokana na makambi yao ya
wagombea urais.,vita hii inatokana na imani kubwa waliyonayo kuwa
ukifanikiwa kusimama ndani ya CCM kama mgombea basi bila kipingamizi
chochote huyo ndie anayekuja kuwa Rais wa Jamhuri kwa awamu ya tano.
Hali ni tofauti kabisa kwa
upande wa Upinzani, kwani kwao hakuna vuguvugu za wagombea Urais na wote
wamejielekeza kwenye majimbo kutokana na ukweli kuwa hakuna tumaini la
kushika dola kwa upinzani. Na hivyo basi vijana wa Chadema, Cuf na NCCR
wamejikita katika kupigania na kuwapambanua wagombea watokanao na
CCM..kwenye bunge la jamhuri wapinzani wanapigana vita ya wagombea wa
CCM, tumbili na wenzake wamejipambanua wazi kuwa wao ni wa kundi moja
wapo la urais ambalo mgombea wake ni wa CCM.,kwenye mitandao ya kijamii
akina Yericko Nyerere hawaandiki tena kuhusu ziara za Babu na mkewe,
wala hawaandiki kuhusu mnyika na porojo zake, hawaandiki chochote zaidi
ya wasifu wa wagombea Urais ndani ya CCM, Kitila Mkumbo na wenzie katika
waandishi waliokuwa wakiibeza CCM kila kukicha wamejikita katika
kuandika Ubora wa wagombea wa CCM, ni ajabu lakini ni kweli kuwa wasomi
hawa ambao wanaona CCM imepoteza dira lakini wanaona katika CCM wamejaa
wenye uelekeo.,ni ajabu.
TanzaniaDaima kama chombo
kikuu cha Chama katika kuripoti taarifa zake, kwa mfululizo tangu mwaka
umeanza front page zake zimejaa wagombea wa CCM na sarakasi zao, Mbowe,
Slaa na Wengineo sio tena ajenda ya wahariri katika chombo hicho.
Inafurahisha, Mbowe amefanya tukio la kuandaa vijana 4000 wa red
brigades na Tanzania Daima imekuja na front page news “HUKU LOWASA, KULE
MWIGULU” Ikasema >wabunge 150 CCMwampigia debe lowasa, yeye
amwachia Mungu., >utafiti wamuibua Mwigulu kuwa Kinara wagombea
Vijana. Hii ni raha ya roho.
Hali hiyo ni kielelezo cha
ukweli kuwa Vijana ndani ya Chadema na Ukawa kwa ujumla wamepoteza
matumaini na vyama vyao na viongozi ndani ya vyama vyao, hawawaongelei
tena wala hawawafikirii kuwa wanaweza kuwa ni Viongozi wa Jamhuri yetu
ya Tanzania. Zamani kidogo matumaini yalikuwepo tena makubwa, tuliamini
kuwa Slaa anaweza kuchukua nchi,tuliamini CCM wameshinda kwa kuiba kura
na kupitisha makontena ya karatasi za kura. Vijana tuliimba wimbo wa
matumaini mapya, hata mimba ya mke wa Slaa kwetu ilikuwa ni ajenda, kuwa
Babu ni Kidume haswaa. Leo hali ni tofauti, Tafiti hazitaji tena kuwa
wapo wapinzani wenye nguvu, Tafiti zinasema CCM maarufu, zinataja orodha
ya wanaCCM tu katika wanaodhaniwa kumrithi JAKAYA, hawatajwi wapinzani.
Hii ni HALI HALISI.,na hizi ndizo salamu zangu kwenu kwa mwaka 2015..JIPANGENI.
|
0 comments:
Post a Comment