Monday, February 23, 2015

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dkt. Shukuru Kawambwa (kushoto)akimsikiliza kwa makini Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) Dkt.Primus Nkwela wakati alipokuwa akimfafanulia jambo alipokuwa mgeni rasmi kwenye hafla ya uzinduzi wa jengo jipya la Mitihani lililopo makao makuu ya ofisi hiyo Mikocheni jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) Dkt.Primus Nkwela ( aliyesimama) akifafanua jambo mgeni rasmi Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dkt. Shukuru Kawambwa (kushoto) wakati hafla ya uzinduzi wa jengo jipya la Mitihani lililopo makao makuu ya ofisi hiyo Mikocheni jijini Dar es Salaam,mwishoni mwa wiki.Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Consolata Mgimba.
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dkt. Shukuru Kawambwa (katikati)akikata utepe kuashiria uzinduzi wa jengo jipya la Mitihani la Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi(NACTE) kutoka kushoto ni Katibu Mtendaji wa (NACTE) Dkt. Primus Nkwela,Kamishina wa Elimu Profesa Uestella Bhalalusesa,Naibu Katibu Mkuu wa Wizara wa wizara hiyo Consolata Mgimba na Mwenyekiti wa barabaza la Taifa la Elimu ya Ufundi Mhandisi Steven Mlote.Hafla hiyo ya Uzinduzi ilifanyika katika makao makuu ya ofisi hizo Mikocheni jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

0 comments:

Post a Comment