Thursday, April 16, 2015

Mwanamuziki Chigwele Che Mundugwao enzi za uhai wake.
MWANAMUZIKI maarufu wa nyimbo za asili nchini, Chigwele Che Mundugwao amefariki dunia leo asubuhi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam alipokuwa amelazwa akisumbuliwa na matatizo ya damu.
Marehemu Chigwele Che Mundugwao amewahi kulipatia taifa sifa kimataifa katika nchi za Scandinavia ambako alijipatia mialiko mbalimbali ya kuwaburudisha mashabiki wake wa muziki.
Miongoni mwa bendi ambazo amewahi kuimbia ni pamoja na Tatu Nane.
Marehemu Che Mundugwao aliyezaliwa mwaka 1968 amefariki akiwa na umri wa miaka 47.

0 comments:

Post a Comment