Thursday, June 18, 2015

Mwanamke mmoja nchini Nigeria ametangaza kupitia
 redio kuwa anatafuta mume, akisema atampa gari na 
nyumba. Mamia ya wanaume walifurika kituo cha radio
 cha Freedom, mjini Kano ambapo polisi walilazimika
 kuitwa kutuliza watu. Msichana huyo, Zainab
 Abdulmalik, 22, amesema alikuwa amekasirishwa mno 
na 'boyfriend' wake wa zamani. Mtangazaji wa redio - Nasiru Zango- ameiambia BBC kuwa Zainab alichagua mchumba kutoka katika mlolongo mrefu wa wanaume waliokuwa wamejipanga nje ya kituo cha redio na kuondoka.

0 comments:

Post a Comment