Wednesday, July 15, 2015

Uongo ukiachwa ukasemwa sana bila kusahihishwa unaweza kugeuka kuwa ukweli.

Tungependa kusahihisha propaganda nyepesi zinazoendelea kuenezwa ili kuusaidia umma usiendelee kupotoshwa kwa mambo yasiyokuwa ya msingi huku kukiwa na mambo makubwa yanayohitaji 'attention' ya Watanzania kuamua mustakabali sahihi wa nchi yao kwa kuchagua MABADILIKO kupitia uchaguzi wa kihistoria hapo Oktoba 25.

1. Zipo taarifa zinaendelea kuenezwa kuhusu makada wa CCM wakiongozwa na Edward Lowassa kuwa wana mpango wa kuhamia CHADEMA. Hadi sasa tunaziona habari hizo kupitia mitandaoni na kwenye vyenye mainstream media. Bila shaka wenye taarifa sahihi za mipango hiyo ni hao hao wanaozieneza. Nasi hatuwajibiki kabisa kuwasaidia kutoa uhakika wa uenezi huo wanaofanya kwa maslahi wanayoyajua.  


0 comments:

Post a Comment