Posted by Williammalecela.com on Saturday, October 03, 2015
 |
Magufuli amnanga Lissu kwao
Amwita mtukanaji na mkwamishaji miradi ya maendeleo
Diana Chilolo amgeuka lowasa asema hana washauri,
DR Magufuli Alisema Lissu hapaswi kuchaguliwa tena kwa sababu
ameshindwa kuwasaidia wananchi wa jimbo hilo kupata maendeleo ya kweli
kwa kushindwa kusimamia miradi mingi ya jimbo hilo kutokana na misimamo
yake iliyochangia kuwaumiza wapigakura wake.
Ninasema wana Ikungi
na Watanzania kwa ujumla tunahitaji kujenga nchi kwa kutumia rasilimali
zetu ambazo zitamnufaisha kila Mtanzania, ila kwa hapa kwenu mmeteseka
kwa sababu ya aina ya mbunge mliyemchagua. Ni bora kukosea jambo lingine
au hata kuoa lakini sio kuchagua, kwani haya ndiyo yanawafanya mteseke.
Mnachagua mbunge ambaye kazi yake ni kuwatukana mawaziri na hata
zinapojadiliwa bajeti wanatoka nje.
“Waziri naye ni binadamu,
hana moyo wa chuma wa kuvumilia matusi, je, kwa hali hii anaweza kuleta
maendeleo kwenu. Hapana msifanye makosa kwa kuchagua wabunge wa matusi
na kutoka nje,” alisema Dk. Magufuli
|
0 comments:
Post a Comment