Friday, October 23, 2015



            

MCHUNGAJI wa kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima aliyejipapambunua kuunga mkono mabadiliko asiyoyajua ya UKAWA, kabla haujafanyika uchaguzi mkuu Jumapili, mwishoni mwa wiki hii miongoni mwa propaganda zao zimeanza kuthihiri uongo.



Watu hawa ambao moja kati ya ahadi zao ni kuwaleta binadamu wenzetu waliotangulia mbele ya haki hadharani wakati familia zao wanaamini wamekufa, wiki hii ni walikuwa miongoni kwenye mazishi ya aliyekuwa mwenyekiti mwenza wa UKAWA, Bw. Emmanuel Makaidi.

Kwa nini?


Kama wangekuwa na uwezo wa ufufuo, wangeanza na kiongozi wa nafasi nyeti katika umoja, lakini wameshindwa na jambo hili ni wazi ni kuwa ni majaribu ya mwenyezi Mungu, tukiomba Watanzania watupishilie mbali na aina hii ya uongozi.

Dura za kisiasa zikionyesha CCM kushinda kwa kishindo na kustaajibisha watu, hiyo kutokana na mgombea wake ambaye yupo jijini Dar Es Salaam kwa siku tatu huku jijini Mwanza ambayo ndiyo ngome kuu ya kura za  Jamhuri wa Muungano wa Tanzania kutokana na idadi yake ya watu, UKAWA wamekuwa wakijiaminisha tu bila takwimu zozote watashindaje.

Leo katika habari hii, tutamalizia pia sehemu ya pili ya Edward Lowassa na mchungaji Gwajima, kwa vile sitakuwa na muda tena wa kuwazungumzia baada ya Jumapili, Lowassa kurejea Monduli moja kwa moja.


Atarejea kwa sababu ndani ya CHADEMA hana cheo chochote na si mtendaji wa aina yeyote wa shughuli za kila siku, hivyo hatakuwa na sababu tena za kwenda ofisi za CHADEMA alizoingia kwa siku moja tu, hadi leo hana sababu ya kuingia tena ofisi hizo.

Hiyo pia itakuwa kwa Mzee wangu Kingunge Ngombale Mwiru, Khamis Mgeja, Makongoro Mahanga, Lembeli na Ester Bulaya ambao watabaki kutumiwa posho tu na Lowassa kama shukrani za kumuunga mkono lakini CHADEMA haina kazi nao tena, natanguliza pole zangu nyingi kwenu.


Leo nikiamini Gwajima aliijua mipango ya upinzani muda mrefu kiasi alipata jeuri ya kumkutana Kardinal Polycap Pengo, iliyomfikisha kwenye matatizo aliyonayo mahakamani kwa sasa.

KIVIPI ? Edward Lowassa ambaye katika mikutano yake ya kampeni ameshindwa kuwaeleza Watanzania aina ya mabadiliko atakayoyaleta na jinsi gani atauondoa umaskini anaoupigia jaramba, ni maigizo kama yalivyokuwa kwa Josephat Gwajima alipokamatwa na polisi kuigiza anaumwa na kulazwa TMJ ili kupata huruma za waumini wake.


Marafiki hawa wanaoshabihiana kwa uigizaji na pia matamshi yao kama nilivyobainisha sehemu ya kwanza, sasa kwa wenye akili timamu tunagundua kwa nini Askofu Gwajima alipata jeuri ya kumtukana Askofu Polycap Pengo. Ana kesi mahakamani ya kujibu, hivyo Lowassa anaposema imefikia wakati sasa Walutheri kutoa Rais, maana yake kesi ya Gwajima itakwisha. Na itakwisha kwani Lowassa akiwa ameshatangaza kuwatoa jela akina Nguza Viking na mwanae Pappii Kocha, kivipi asiweze kuiondoa mahakamani kesi ya  Gwajima kumtukana Pengo.


Kwa mantiki hiyo kujiaminisha kwao hadi alitukana ni kwamba si lazima wapate kura za dhehebu la  Roman Catholic ambako Askofu wao Pengo alishaambiwa “ Amekula maharage eeh…aah mpuuzi mmoja… mjinga mmoja, asiyefaa mmoja !.



Kwa, wanaoongozwa na Kardinal Pengo lazima wajitafakari inakuwaje aliyemtukana kiongozi wao, sasa anapanda jukwaani na  Lowassa wakiitaka nchi kwa kuzungumzia dhehebu moja tu kati ya Wakristo lukuki. Kama ubaguzi kwa Wakristo wenyewe kwa wenyewe umefikia hapo, vipi kwa Waislam?


Maigizo haya yatatupeleka tusikotarajiwa, Watanzania kweli tunataka nchi ibadilike iende na wakati kutokana na Dunia inavyokimbia kwa sasa, lakini mabadiliko yanaanza kwetu wenyewe, tusome na kupata uelewa mkubwa wa mambo ya Dunia na kukimbizana na soko la ajira, pia tufanye kazi kwa bidii.

Si kweli, Machinga anayeuza maji Kariakoo akiingia Lowassa madarakani mwaka huo huo, maisha yake yanakuwa tambalale. HAIWEZEKANI ASUBUHI UUZE JUISI KWENYE NDOO YA MAJI JIONI UKAKAE KITI KIREFU UNAKUNYWA BIA, UTAENDELEA KWA MTAJI UPI ?


Wapo walioendelea kwa kujisomesha na wapo walioendelea kwa kuuza juisi kwenye ndoo ya maji hatimaye wakapata vioski vikubwa vya kuunza vinywaji baridi hadi kufikia kujenga nyumba. Wamefanya kazi na kujiwekea malengo, hivyo kufanya kazi kwa bidii ni mabadiliko tosha ya maisha yako ya sasa ulipofikia.

Tunahitaji mabadiliko, halafu nini kinafuata ama kitafuata tu baada ya mabadiliko ? Nchi haisimami, dunia inasonga mbele tutasimama wakigombea madaraka kwenye mabaraza ya mawaziri, wakimaliza watagombea ukuu wa mikoa, wilaya na makatibu wakuu hiyo ni miezi mitatu kama si sita.


Narudia tena genge lililomzunguka Lowassa kutaka kuingia IKULU la Gwajima na wengineo ni tatizo ambalo heri mara 100 ya CCM mzee. Ndio maana CHADEMA badala ya kumfanyia kampeni Lowassa kwa wakati huu wanapambana kumsafisha, huku wasishaji wenyewe wakiwa wachafu mikononi, usoni na mioyoni mwao.

OMBI langu kwa Watanzania walioweka nadhiri ya kukaa vituoni kulinda kura kama kweli wanafikiri wataibiwa na wanaamini hivyo, wafuate ushauri huu;


CHA KUFANYA;  UKISHA PIGA KURA ILI UILINDE VIZURI KURA YAKO USIKUBALI KUIDUMBUKIZA KWENYE KISANDUKU, BAKI NAYO ILI USIIBIWE UKIWEZA MPELEKEE MHUSIKA ALIYEKUSHAWISHI UBAKI KUILINDA ILI UMWONYESHA UNAYO HAIJAIBIWA.


Tutafakari sana kila tunalolilisikia tulipime sana, Mtanzania tusikurupuke, nchi ipo mikononi mwako. Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Afrika.

Le Mutuz Nation



0 comments:

Post a Comment