Barnaba afanya kazi na msanii mwingine wa Uganda, Kleyahâ
Wawili hao wanarekodi wimbo uitwao Msobe Msobe
katika studio za High
Table zinazomilikiwa na Barnaba. ,Kleyah alinitafuta kupitia simu alipewa namba
yangu kupitia kituo kimoja hivi cha redio. Ni msanii ambaye mwenye uwezo
mkubwa sana na sikutegemea kama msanii kama huyu anaweza kunitafuta
maana nilimfutilia nikaangalia biography yake ipo vizuri, lakini
aliniamini na ndio maana tukafanya kazi. Nimemuimbisha Kiswahili humo
ndani vizuri ameimba.
Kleyah ni msanii aliyezaliwa nchini Uganda na kuchukua elimu yake ya juu
katika masuala ya mawasiliano katika chuo cha Phoenix nchini Marekani.
Kwa sasa Kleyah anaishi nchini Tanzania akiwa anatarajia kukamilisha
masomo yake ya utawala wa kimataifa (Degree in
International Management).

0 comments:
Post a Comment