Mwanamume mmoja kutoka Australia amevunja rekodi ya kutumia mataa mengi zaidi kwenye mti bandia wa Krismasi.
Kitabu
cha kuweka rekodi zinazotambuliwa kimataifa cha kampuni ya Guinness
World Records, kilithibitsha kuwa Bwana David Richards, alitumia mataa
zaidi ya 8,838 kwenye mti mrefu bandia wa chuma ambapo mataa yake yote
yalimeremeta.
Mti huo wenye urefu wa mita 22 uliwekwa katika mji wa Canberra.
Watu
wa kujitolea kukiwemo mhandisi wa umeme, mhandisi wa ujenzi,
wachomeleaji wa vyumba, maseremala, waashi, na watungaji wa vyuma ni
baadhi ya watu waliomsaidia katika kampeni hiyo yake ya kuvunja rekodi
ya dunia.
0 comments:
Post a Comment