AWACHA KWA CHAFUKA! WATUPIANA MATUSI YA NGUONI.
KUMBE MARIAM MSABAHA MCHAGA???
16th Nov 2015 02:10 am
KUMBE MARIAM MSABAHA MCHAGA???
16th Nov 2015 02:10 am
Wanakisima Jinamizi la ukabila juu ya
upatikanaji wabunge wa viti maalum ndani ya BAWACHA bado laendelea
kulitesa baraza hilo linalo ongozwa na Halima Mdee.
Hamida anayetajwa katika majibizano haya
ya whatspp ndio kiongozi pekee wa BAWACHA ambaye si mbunge wa viti
maalum. Hamida ni makamu mwenyekiti wa BAWACHA upande wa Zanzibar na
alipata nafasi hiyo baada ya kumshinda Maryam Msabaha.
Inasemekana ama waweza kusema kuna
tuhuma kuwa kigezo kikubwa cha kupata ubunge wa viti maalum ndani ya
CHADEMA aidha uwe karibu na viongozi wa kitaifa chama hicho(kimapenz) au
uwe mchaga.
Maryam Msabaha ni mchaga, na kama majibizano hayo yanavyo jieleza, kwao kaskazini kwanza Zanzibar baadae!
BAWACHA wanatuhumiana wenyewe kwa
wenyewe, BAWACHA hawapatani, BAWACHA ukabila unawatafuna, BAWACHA viti
maalum vimewavuruga! BAWACHA haijatulia, BAWACHA yahitaji kupepewa!
Baada ya kuvuana nguo katika group lao
la whatspp wakaamua kulifunga na kufungua lingine ambalo wale wenye
vurugu hawatahushwa! Inasemekana kila makundi mahasimu kila moja sasa
limefungua kundi lake, makundi ambayo yabahusisha baadhi ya viongoz wa
waandamizi wa BAWACHA na wabunge wa viti maalum.
BAWACHA waliotemwa wana hasira, sababu
kuna uwezekano mkubwa uchaguzi wa mwaka 2020 tutafanya chini ya katiba
mpya, katiba ambayo haitakuwa na viti maalum, wanawake watatakiwa kwenda
kugombea majimboni, hivyo kwa wale wanawake waoga wa kwenda jimboni
mwaka huu ilikuwa ndio turufu yao mwisho!
Kwahivyo waweza kugundua hasira zao
zimesababishwa na tuhuma za ukabila, lakini pia nafasi hizo hazitakuwepo
tena mwaka 2020. Binafsi naomba heri mwaka 2020 tupate katiba mpya ili
dada zetu waponyeke na viboko vya viongozi wenye sauti katika vyama vya
siasa!
Wanakisima tuendelee kuwa pamoja, hiv
karibuni nitawapa lingine lililotokea BAVICHA na UWT, nina fuatilia
uthibitisho tu wa habari zenyewe, na nikipata sitaacha kuwajuza watu
wangu.

0 comments:
Post a Comment