Linah Sanga amekanusha uvumi kuwa ana ujauzito na kuweka taarifa sawa
kuhusu afya yake ya uzazi
Mwimbaji huyo wa ‘No Stress’ amesema
kuwa kwasasa anajipanga ndio maana hajaamua kupata mtoto lakini
hiyo haimaanishi kuwa ana matatizo yoyote ya uzazi kama badhi ya watu
wanavyohisi
Mimi nipo vizuri bhanaa sina tatizo la uzazi ila huwa najipanga ndio maana watu hawajahi
kuniona nina ujauzito, lakini kwa sasa najiachia sanaa hivyo
muda wowote wanaweza kusikia jambo
alisema Linah kupitia Planet Bongo ya EATV,
Hii si mara ya kwanza Linah kukanusha taarifa za kuwa mjamzito.
Mwaka jana (2014) mwanzoni Linah aliwahi kukanusha taarifa kama hizo, na kusema
maswala ya ujauzito, kuolewa na kuwa na familia ni ya muhimu kwa kila msichana
lakini upande wake muda wa kuvifanya hivyo ulikuwa bado.
0 comments:
Post a Comment