Mayunga
yupo nchini Marekani alikoenda kufanya wimbo na Akon. Wimbo huo ni
sehemu ya mambo anayotakiwa kufanya baada ya kushinda shindano la Airtel
Trace Music Star.
Tayari wawili hao wamesharekodi wimbo huo na kinachofuata sasa ni video ya muziki.
Alhamis hii Mayunga alieleza kupitia Instagram kuwa model
atakayetumika kwenye video hiyo aliwahi kutumika kwenye video ya wimbo
wa Big Sean na Chris Brown.
“Anaitwa @itsssvia unaweza kumtazama katika video ya big sean ft
chris brown alionekana kama mhusika mkuu wa kike na nina furaha kuhusika
katika video yangu kama video queen,” Mayunga aliandika kwenye picha
aliyoiweka Instagram akiwa na msichana huyo.
Viandra anaonekana kwenye video ya wimbo wa Big Sean aliowashirikisha Chris Brown na Ty Dolla $ign ‘Play No Games.’
0 comments:
Post a Comment