Kesi hiyo ya madai iliyofunguliwa Novemba 19, mwaka huu na Magambo Masato na wenzake 30, inapinga matokeo yaliyompa ushindi Bulaya na wenzake 20 pamoja na mkurugenzi wa Wilaya ya Bunda ambaye alikuwa Msimamizi wa Uchaguzi na Mwanasheria Mkuu.
Katika matangazo yaliyowekwa katika ubao wa matangazo ya Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, waomba maombi wanadai upatikanaji wa ubunge wa Bulaya haukuwa halali kutokana na kukiukwa kwa baadhi ya mambo.
Taarifa hiyo ilidai msimamizi wa uchaguzi hakutakiwa kumtangaza Bulaya kuwa mbunge halali wa jimbo hilo kutokana na kwenda kinyume cha sheria pamoja na kanuni za uchaguzi huo.

0 comments:
Post a Comment