Thursday, December 10, 2015

 

Mwenyekiti wa kwanza wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambaye pia Muasisi wa chama hicho, Edwin Mtei, amesema kuwa uamuzi wa Rais Magufuli wa kufuta sherehe za uhuru utakuwa umeleta tija kubwa kwa taifa ambapo miaka mingi taifa limekuwa likichezea mabilioni ya shilingi bila faida kwa taifa.

Mtei amesema kuwa sherehe hizo zilizokuwa zikifanyika kwa shamrashara  zilikuwa zinagharimu fedha za walipa kodi kwa anasa za kula,kunywa na kulewa huku watanzania wakikosa huduma muhimu.

0 comments:

Post a Comment