Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASCO , Mhandisi Cyprian Luhemeja akishirikiana na wafanyakazi wa DAWASCO katika zoezi la usafi kwenye soko la Kariakoo katika maadhimisho ya siku ya Usafi kitaifa.
Shirika
la majisafi na majitaka Dar es salaam(Dawasco) katika kutekeleza agizo la mh.
Rais john pombe magufuli la kuadhimisha sherehe za uhuru kwa kufanya usafi
katika maeneo mbalimbali, leo DAWASCO imefanya usafi katika soko kuu la
kariakoo lilipo wilaya ya ilala, jijini Dar Es Salaam, ikiwa ni jitihada za kupambana na ugonjwa wa
kipindupindu ulioenea nchi nzima.
Usafi
huo uliongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mh Mecky Sadick pamoja na
Mkurugenzi Mkuu wa DAWASCO Mhandisi Cyprian Luhemeja ulifanya usafi katika
maeneo yote muhimu ikiwemo sokon Shimoni, Mtaa wa Msimbazi na Uhuru pamoja na
uzibuaji wa Mitaro ya Majitaka katika Mitaa ya Libya na Zanaki.
Akiongea
katika usafi huo Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam alisema usafi ni jukumu la kila
mwananchi bila kujali itikadi yake na hivyo kuwahimiza wananchi kuwa na tabia
ya kufanya usafi katika maeneo yao kuliko kusubiri kupewa maagizo na serkali.
Kwa
upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASCO alisema siku hiyo wameiadhimisha kwa
kufanya usafi katika soko la Kariakoo ambalo ni moja ya wateja wake ili kuwa
mfano mzuri kwa wananchi na jamii nzima inayohudumiwa na Soko hilo.



0 comments:
Post a Comment