Friday, December 25, 2015

prime india
Wakati huo huo Waziri Mkuu wa India Narendra Modi ametua nchini Pakistan kwenye ziara ya kushtukiza ambapo amekutana na mwenzake Nawaz Sharif.

Bw Modi alikuwa safarini kurejea India kutoka Afghanistan alipoamua kutua katika mji wa mashariki wa Lahore. Ziara yake imelingana na siku ya kuzaliwa ya Bw Sharif.
Bw Modi ndiye waziri mkuu wa kwanza wa India kuzuru Pakistan tangu 2004.
Mataifa hayo yamepigana vita mara tatu tangu kujipatia uhuru kutoka kwa Uingereza, vita vivili kuhusu jimbo la Kashmir, kila moja likidai umiliki wa eneo lote la Kashmir, mgogoro uliodumu kwa zaidi ya miaka 60 sasa.

0 comments:

Post a Comment