Naibu Waziri wa
Kilimo,Mifugo na Uvuvi William Ole Nasha amesema kuwa hatamwangusha
Raisi John Pombe Magufuli na Watanzania kwa kuhakikisha kuwa anawajibika
na kufanya kazi kwa bidii na kuleta mabadiliko katika sekta hizo .
Nasha ambaye uteuzi huo
ulivyotangazwa rasmi kwenye vyombo vya habari ulimkuta katika Baraza la
Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro hali iliyowashangaza
wengi kwani hawakuwa wametarajia kuwa uteuzi huo ungetokea.
Akizungumza katika baraza la
Madiwani Nasha alishukuru kwa uteuzi huo na kuahidi kuwa hatawaangusha
Watanzania kuwa hana rekodi ya kukosa maadili.
“Umakini mkubwa umetumika kuteua
baraza la Mawaziri mpaka leo hii Mheshimiwa Raisi hajamaliza kuteua
baraza , ni heshima kubwa sana kwangu namshukuru Magufuli kwa dhamana
hii kubwa “ Alisema Nasha

0 comments:
Post a Comment