Tuesday, December 22, 2015

Mkuu Mpya wa mkoa wa Kilimanjaro Mh. Amosa Makalla alipofanya ziara kustukiza uwanja wa Ndege KIA sasa hivi. Amewapongeza uongozi wa KADCO, wafanyakazi na vyombo vya Ulinzi kwa kukamata nyara za serikali na utoroshaji wa madini ikiwa ni utekelezaji wa maagizo aliyoyatoa trh 24 November mwaka huu kuwa uwanja huo isiwe uchochoro wa madawa ya kulevya, madini na nyara za serikali . Raia watatu kwa matukio matatu wameshakamatwa kwa kutaka kutorosha madini na nyara za serikali
Ameagiza menejimenti kuwaweka pembeni watumishi 6 wa Kadco walilo husika na kusaidia watuhumiwa katika matukio matatu ambao kwasasa kesi zao zipo polisi kwa uchunguzi.

Mkuu Mpya wa Mkoa wa Kilimanjaro Mh. Amos Makalla akizungumza na watendaji wa Uwanja wa Ndege wa KIA baada ya kuwashitukizia ghafla muda mchache uliopita.






0 comments:

Post a Comment