Waziri
wa wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo ameuagiza uongozi wa
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Kanda ya Ziwa kuhakikisha
wanauingiza mkoa wa Kagera katika Gridi ya Taifa baada ya kubainika nchi
inaingia gharama kubwa kununua umeme kutoka Uganda.
Alitoa
agizo hilo jana wakati wa ziara yake ya kikazi mkoani Kagera na
kusisitiza katika mipango mipya ya Tanesco kwa sasa, ni lazima iondokane
na umeme wa gharama kubwa.
Katika
ziara hiyo ambayo alikagua mitambo ya kusambaza umeme katika wilaya za
Bukoba, Biharamulo na Ngara, Muhongo alisema umeme unaonunuliwa kutoka
Uganda wa megawati 5.2 , kila uniti hununuliwa senti nane za Kimarekani.
Aliagiza
kwamba kabla ya Tanesco kusaini mkataba mpya na Uganda, wanapaswa
kusaini mkataba wa muda wakati wakiendelea kuweka utaratibu wa
kuhamishia mkoa wa Kagera kwenye Gridi ya Taifa. Alisema mkoa huo
ukiingizwa kwenye gridi, Tanesco itaepuka gharama kubwa za kunununua
umeme wa gharama ya juu kutoka nchi hiyo.
Alisema
kwa sasa Gridi ya Taifa imefika Nyakanazi, wilayani Biharamulo. “Kwa
hiyo hata wilaya nyingine hazina budi kuingizwa katika gridi ili kufanya
mkoa uwe na umeme wa uhakika na wa bei nafuu utakaowafanya wananchi
kuzalisha kwa kutumia umeme…,” alisema.


0 comments:
Post a Comment