Tuesday, December 22, 2015




MKUU wa Polisi nchini Inspekta Jenerali (IGP) Ernest Mangu amekanusha kufutwa kazi kwa askari kadhaa wanaodaiwa kuwa na vyeti feki kama iliyosambazwa kwenye mitandao ya kijamii juzi na akasema Jeshi lake linamtafuta mtu ambaye amesambaza taarifa hizo alizoita za uzushi.

IGP Mangu alisema jana kuwa taarifa hizo sio za kweli na jeshi lake halikusambaza taarifa hizo hivyo wanamtafuta kwa udi na uvumba mtu aliyesambaza taarifa hizo za uwongo na akajifanya ni Jeshi la Polisi.

“Taarifa hizo sio za kweli na tayari msemaji wa Polisi jana (juzi) alishazikanusha kupitia hiyo mitandao ya kijamii.Nasisitiza kuwa tunamsaka aliyesambaza taarifa hizo za uwongo,” alisema IGP Mangu wakati anajibu maswali ya waandishi wa habari jana.

Juzi kwenye mitandao ya kijamii kulipositiwa majina ya askari Polisi wengi wenye vyeo vya chini na vya kati wakidaiwa kuwa wamefukuzwa kazi baada ya kubainika kuwa walijipatia ajira hiyo kwa kutumia vyeti bandia.

0 comments:

Post a Comment