Friday, December 4, 2015

<br />
<br />
Rais John Magufuli

Rais John Magufuli

Mwanza. Chama cha Albino Tanzania (Tas) Mkoa wa Mwanza, kimemuomba Rais John Magufuli atumie nafasi zake kumi za uteuzi kuchagua wabunge wenye ulemavu  ili Bunge liwe na sauti ya kuwatetea.



Mwenyekiti wa Tas mkoani hapa, Alfred Kapole alisema juzi kuwa ili sauti za watu wenye ulemavu zisikike kwa nguvu ni vyema Bunge likawa na wabunge wengi wenye ulemavu.



“Tunamwomba Rais Magufuli kupitia nafasi zake 10 za uteuzi wa wabunge, ateue wabunge wenye ulemavu ili na sisi matatizo yetu yawakilishe na kusikika kwa nguvu kubwa tofauti na ilivyo sasa,” alisema Kapole na kuongeza:









“Tunapata tabu kwenye miuondombinu iliyopo, tunaomba hili nalo aliangalie kwani walemavu tumekuwa tukipata shida hasa tunapohitaji huduma kwenye baadhi ya ofisi.”



Vilevile, Kapole alisema wanafahamu kuna hukumu zilizotolewa kwa watu waliohusika na mauaji ya albino,  lakini hazijatekelezwa, hivyo wanamwomba Rais kushughulikia kwa kina.



Katibu Mkuu wa Shirikisho la Vyama vya Watu wenye Ulemavu Tanzania (Shivyawata), Felician Mkude alisema albino wanahitaji uangalizi  kwani wamekuwa wakiuawa kwa imani za kishirikina na kwamba vitendo hivyo vimekuwa vikiongezeka siku hadi siku.



“Vitendo hivyo kwenye makaratasi vinaonekana vinapungua, lakini vinaongezeka kila siku, tunavyoviona haviripotiwi kwa wingi,”  alisema  katibu huyo.

Source;Mwananchi



0 comments:

Post a Comment