Rais Barack Obama amesema Marekani haitayumbishwa na shambulio la Jumatano katika mji wa San Bernardino, California.
"Sisi
tuna nguvu. Tuko imara," amesema kwenye hotuba yake ya kila wiki
kupitia redio, akisema inawezekana kwamba watu wawili waliofyatua risasi
na kuua watu 14 katika mji huo walikuwa wameingizwa kwenye itikadi
kali.
Syed Rizwan Farook, 28, na mkewe Tashfeen Malik, 27,
walitekeleza mauaji hayo kabla ya kuuawa kwenye ufyatulianaji wa risasi
kati yao na polisi.
Aidha amefahamika kuwa FBI wanachunguza kisa hicho kama kitendo cha ugaidi.
Kundi
la wapiganaji wanaojiita Islamic State Jumamosi lilisifu shambulio hilo
na kusema lilitekelezwa na “watu wawili wanaounga mkono Islamic State".
Taarifa
hiyo iliyopeperushwa kupitia redio ya IS ya al-Bayan haikutoa ishara
zozote kuhusu kuhusika kwa kundi hilo kwenye shambulio hilo katika
sherehe ya Krismasi kituo cha Inland Regional Center.
"Tunajua
kuwa Islamic State (IS) na makundi mengine ya kigaidi yanawahimiza watu – kote
duniani na hata nchini mwetu – kutenda vitendo vibaya vya mauaji, wakati
mwingine,” Bw Obama amesema.
"Sote, serikali, idara za
usalama, jamii, viongozi wa kidini, tunahitaji kufanya kazi kwa pamoja
kuzuia tusipotoshwe na itikadi hizi za chuki.”


0 comments:
Post a Comment