
Waziri
wa Katiba na Sheria, Dk Harrison Mwakyembe amesema Rais amempa kazi ya
kuhakikisha anakamilisha mchakato wa Katiba Mpya pamoja na uanzishwaji
wa Mahakama ya Rushwa.
Kura
ya Maoni ya kupitisha Katiba Inayopendekezwa ilipangwa kufanyika Aprili
30, lakini Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ikatangaza kuiahirisha hadi
itakapotangazwa tema, ikisema inataka kukamilisha kwanza uandikishaji
wapigakura kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 25.
Lakini
kabla ya kutangaza kuahirisha kazi hiyo, vyama vya upinzani, ambavyo
vilisusia Bunge la Katiba kwa madai kuwa lilikiuka utashi wa wananchi
kwa kuweka kando sehemu kubwa ya mapendekezo yaliyokuwa kwenye Rasimu ya
Katiba, walikuwa wakitaka mchakato huo uanze upya.
0 comments:
Post a Comment