Haijalishi
kama utaweza kuiongea kwa ufasaha au hukumbuki hata neno moja, lugha ya
kwanza uliyojifunza ukiwa mtoto imeshaubadili ubongo wako kiasi ambacho
hakuwezi kuwa na mabadiliko tena.
Watafiti wa nchini Canada wamebaini kuwa kusikia lugha ya kwanza enzi
za utoto kunaathiri ubongo wa mtu na jinsi anavyokabiliana na lugha
nyingine miaka mingi baadaye.
Hii hutokea hata kwa wale ambao hawajazungumza lugha yao ya kwanza
katika maisha yao yote na hata kwa wale wanaomini kuwa wameisahau
kabisa.
Watafiti wa McGill University and the Montreal Neurological Institute
walifanya utafiti katika makundi matatu ya watoto wenye umri wa miaka
10 na 17 wenye historia mbalimbali za lugha.
Kundi moja liliundwa na watoto waliozaliwa na kukulia wakizungumza Kifaransa.
Watoto kwenye kundi la pili walikuwa wanazungumza Kifaransa na
Kichina na la tatu liliundwa na watoto wa Kichina walioasiliwa kwenye
familia za Kifaransa kabla hawajafikisha miaka mitatu na hawajawahi
kuzungumza tena Kichina.
Watoto wote waliambiwa kutamka maneno sawa ya Kifaransa ambayo hayakuwa na maana yoyote kama ‘vapagne’ au ‘chansette.’
Wakati wa utafiti huo, watafiti walitumia kile kinachoitwa
‘functional magnetic resonance imaging’ (fMRI) kutazama maeneo yapi ya
ungo yametumika.
Pamoja na makundi yote kufanya vizuri, fMRI ilibaini kuwa baadhi ya
makundi yalikuwa tofauti kuhusiana na upande upi wa ubongo uliotumika.
0 comments:
Post a Comment