Posted by Williammalecela.com on Tuesday, January 19, 2016
Hivi karibuni kumezuka mjadala mpana
kwenye mitandao ya kijamii hasa kwa wapenzi wa burudani nchini, baada ya
vyombo mbalimbali vya habari kuripoti kuwa Diamond Platnumz anauwezo wa
kuidhinisha upigwaji wa vichupa wa wasanii wa Bongo kwenye kituo cha
MTV na akiamua zisipigwe anaweza kufanya hivyo.
Mjadala huo ulifika mbali mpaka
kumuhusisha nguli huyo wa Afro Pop kuwa yeye ndiye kizuizi kikubwa cha
nyimbo za msanii Alikiba kupigwa katika kituo hicho kikubwa cha MTV.
Kwa upande wake Alikiba baada ya kupata
taarifa za kuwa Diamond ndiye anahusika katika kuidhinisha uchezwaji wa
video za wasanii wa Bongo amefunguka na kueleza kuwa kama ni kweli MTV
watakuwa wanakosea, kwa sababu wasanii wa ndani wanafanya vichupa vikali
vinavyo wagharimu, hivyo akitokea mtu kuzibania inakuwa sio kitu
kizuri.
Kwa upande wa Menejimenti ya Diamond
Platnumz wamelizungumzia suala hilo na kueleza kuwa, halina ukweli
wowote bali watu walimuelewa vibaya Diamond Platnumz kipindi anaelezea
suala la mchango wake kwa wasanii wa ndani, katika mahojiano yake na
mtangazaji wa kipindi cha Papaso Dijaro Arungu cha TBC FM.
Menejimenti ya Diamond Platnumz
imeongeza na kueleza kuwa kama Diamond angekuwa anatoa idhini ya
uchezwaji wa video za wasanii wa ndani, basi nyimbo za wasanii
waliokaribu na Diamond zingepigwa huko kwa mfano Harmonize, Yamoto Band,
Madee na wengineo.
0 comments:
Post a Comment