Naibu
spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dokta Tulia Ackson
ameyata madhehebu ya dini nchini kuendelea kuliombea taifa na viongozi
wake ili waweze kuwatumikia watanzania kwa usawa na uadilifu pamoja na
kuliombea taifa mungu aliepushe na janga la kipindupindu linaloikabili
baadhi ya mikoa ikiongozwa na mkoa wa Morogoro.
Dokta Tulia ametoa wito huo mjini Morogoro wakati wa kumtunuku tuzo
ya Heshima askofu mkuu wa kanisa la TAG Dokta Barnabas Mtokambali kwa
kutambua mchango wake wa maendeleo katika jamii tuzo iliyotolewa na
shirika lisilo la kiserikali la Weis Man la hapa nchini ambapo Dokta
Tulia amesema jitihada zilizofanyika kuliombea taifa wakati wa uchaguzi
mkuu mwaka jana ziendelee kwani viongozi wanawakati mgumu wa kuhakikisha
Tanzania inakua kiuchumi.
Akipokea tuzo hiyo askofu mkuu wa TAG askofu Dokta Barnabas
Mtokambali ameshukuru shirika hilo kwa kutambua umuhimu wake katika
kusaidia jamii ambapo kufuatia mkoa wa Morogoro kuongoza kwa kuenea kwa
kasi ugonjwa wa kipindupindu askofu Mtokambali amewataka wananchi
kuzingatia kanuni za usafi wa mazingira na chakula ili kutokomeza
mlipuko huo.
Katika misa hiyo naibu spika Dokta Tulia Ackson ameshiriki maombi
ya kuliombea bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linalotarajia
kuanza mapema Januari 26 mwaka huu.
0 comments:
Post a Comment