Waziri wa ujenzi uchukuzi na mawasiliano prof.MAKAME MBARAWA ,
amewataka makandarasi wanaojenga barabara za MANGAKA MTAMBASWALA na
MANGAKA NAKAPANYA zilizopo katika wilaya ya NANYUMBU mkoani MTWARA ,
kuongeza kasi ya ujenzi ili kuhakikisha barabara hizo zinakamilika kwa
wakati na kwa ubora unaotakiwa .
Prof.MBARAWA ametoa wito huo mkoani MTWARA mara baada ya kutembelea
barabara hizo zenye jumla ya kilometa miamoja thelathini na mbili,
zinazojengwa kwa kiwango cha lami na kueleza kutoridhishwa na kasi ya
utekelezaji wa miradi hiyo, ikilinganishwa na muda uliobaki kwa mujibu
wa mikataba yao na serikali.
Akiwa katika Wilaya ya NANYUMBU , waziri MBARAWA ametembelea mradi
wa barabara ya MANGAKA MTAMBASWALA nyenye jumla ya kilometa sitini na
tano nukta tano, ambapo mhandisi mkazi wa mradi huo ANORD MSENGEZI
amemueleza waziri huyo kuwa hadi sasa ujenzi umekamilika kwa asilimia
arobaini na tano.
Aidha prof. MBARAWA pia ametembelea mradi wa barabara ya MANGAKA
NAKAPANYA yenye urefu wa kilometa sabini nukta tano na kuelezwa kwamba
hadi sasa ujenzi wake umekamilika kwa asilimia hamsini na tatu.
Kwa upande wake meneja wa wakala wa barabara TANRONDS mkoa wa MTWARA
mhandisi AISHA SALIM amesema wakala huo utafuatilia na kusimamia kwa
karibu makandarasi hao, kuhakikisha wanakamilisha ujenzi huo kwa wakati
na kwa ubora unaotakiwa.
0 comments:
Post a Comment