Saturday, January 2, 2016



 
Halfa ya kuapishwa kwa makatibu wakuu na naibu makatibu wakuu 26 iliyofanyika jana Ikulu Jijini Dar es Salaam ilikuwa ya aina yake kutokana na kuapa mara mbili, huku Rais John Magufuli akiwaeleza kuwa asiyeweza kazi  aseme asile kiapo, akae kando.

“Inawezekana tulizungumza kwa ujumla lakini kumbe si wote wanakubali masharti kuhusu rushwa, kutoa vitu vya upendeleo. Kwa hiyo, niwaombe makatibu wakuu pamoja na kwamba mlishaapa kwangu, ambaye hakubaliani na hilo asimame kando ili waliobaki waendelee,” alisema Rais Magufuli kabla ya kiapo cha pili cha uadilifu. 

Hakuna aliyesema hawezi kazi hivyo wote walikula kiapo hicho.

Baada ya hapo, Balozi Sefue aliwataka kunyanyua mikono yao juu na kusoma kiapo  hicho cha uadilifu kwa sauti: “Mnakula kiapo hiki kulingana na makubaliano, kwamba ukiwa mtumishi wa Serikali lazima ukubali kusaini fomu hii inayoashiria kuwa kiongozi ana dhamana kubwa kwa nchi na wananchi.”

0 comments:

Post a Comment