Posted by Williammalecela.com on Thursday, January 21, 2016
 |
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mh. Amos Makalla amefanya ziara wilaya ya Rombo kwa kuweka
jiwe la msingi mradi wa Maji Ngareni na kuzindua hosteli ya wasichana
sekondari ya Horombo Aidha amefanya kikao cha pamoja madiwani,
watendaji wa kata na Vijiji na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na usalama
Rombo na kuelekeza yafuatayo 1. Amepiga marufuku unywaji wa pombe
kupindukia, unywaji pombe wakati wa kazi na utengenezaji pombe haramu
ikiwemo gongo na nyingine 2. Ameagiza Kamati ya Ulinzi kuimarisha
ulinzi na msako kwa wahalifu wakiwemo majambazi toka nchi jirani ya
kenya na pia wadhibiti wahamiaji haramu wanaopitia mpaka wa Tanzania |
0 comments:
Post a Comment