Tuesday, January 26, 2016

Same kuhusu OPERESHENI MIRUNGI SAME kimefanyika leo kwa kushikirikisha vyombo vya Ulinzi na usalama, madiwani,watendaji wa kata na Vijiji, wenyeviti wa Vijiji na wakuu wa vituo vya polisi
Mkuu wa wilaya ametoa taarifa kuwa siku 28 alizotoa mkuu wa Mkoa tarehe 29 dec 2015 kuwa kila Mwananchi afyeke na kungoa mirungi kwa hiari yake zimekwisha na kwamba katika Vijiji 28, na kata 13 kati ya wakulima ya mashamba 921 yenye ekari 260 ya mirungi ni wakulima/ mashamba 313 tu Sawa na 34% waliotekeleza agizo la mkuu wa Mkoa na Hivyo mkuu wa Mkoa Ameagiza
1. Serikali baada ya siku 5 kuanzia leo imejipanga kufanya operesheni kabambe ya kuhakikisha mashamba yote yaliyobaki yanafyekwa na wananchi watakaokaidi kutekekeza katika siku Tano watakamatwa na kufunguliwa mashitaka na kwa mujibu wa sheria ya madawa ya kulevya adhabu yake ni kifungo miaka 30
2. Ameagiza watendaji, madiwani na wakuu wa vituo vya polisi kuhamasisha wananchi kutumia siku 5 kufyeka na kungoa mirungi yote
3. Wilaya ya Same inaongoza kwa kulima, kuuza mirungi nchini ambayo huuzwa mikoa mingi nchini na nchi jirani ya Kenya na madhara yake ni kuathiri nguvu kazi hasa vijana, utoro mashuleni na kupelekea wilaya ya Same kwa Matokeo ya darasa la saba kuwa na Shule sita za mwisho kimkoa













0 comments:

Post a Comment