Siku
74 baada ya kushindwa katika Uchaguzi Mkuu mwaka jana, Chama cha
Demokrasia na Maendeleo (Chadema) jana kimefanya kikao cha kujitathmini
na kuweka mpango kazi kwa miaka mitano ijayo.
Katika
uchaguzi huo uliofanyika Oktoba 25, mwaka jana, mgombea urais kwa
tiketi ya chama hicho, Edward Lowassa alishindwa na Rais John Magufuli
wa CCM aliyepata kura Milioni 8.8 sawa na asilimia 58.5.
Lowassa
alipata kura Milioni 6 sawa na asilimia 39.97 ya kura zote.Chadema pia
ilipata wabunge 70, wakiwamo 36 wa viti maalumu huku CCM ikipata wabunge
188.
Katika
chaguzi ndogo saba zilizofanyika baada ya uchaguzi huo mkuu, CCM
iliongeza wabunge takribani tisa, wakiwamo wa viti maalumu watatu na
Chadema mbunge mmoja wa kuchaguliwa.

0 comments:
Post a Comment