SERIKALI imewahakikishia Watanzania kuwa mchakato wa kuanzishwa kwa
Mahakama Maalumu ya mafisadi na wezi, umefikia hatua nzuri. Waziri wa
Katiba na Sheria, Dk Harrison Mwakyembe alisema hayo juzi bungeni mjini
hapa, wakati akichangia Hotuba ya Rais ya Ufunguzi wa Bunge.
Akizungumzia mchakato wa kuanzishwa kwa mahakama hiyo maalumu,
Mwakyembe alisema unakwenda vizuri na utakapokamilika Watanzania
watafahamishwa. “Kiongozi wa Serikali ya Awamu ya Tano, akitoa tamko
lazima litekelezwe.
Kama tunakumbuka Rais, kwa nyakati tofauti kipindi cha kampeni,
aliahidi kuanzisha Mahakama Maalumu ya Mafisadi na Wezi,” alisema
Mwakyembe. Akiizungumzia hotuba ya Rais, Mwakyembe alisema ikiachwa
hotuba ya Mwalimu Nyerere, ya Magufuli pia ni bora na iligusa mioyo ya
Watanzania wenye nia njema na Taifa.
“Wakati rais anatoa hotuba yake iliyokuwa na aya 160, alipigiwa
makofi na vigelegele mara 137, ni zaidi ya asilimia 86, ya Dk Martin
Luther ambaye ni Mmarekani mweusi,” alisema na kuongeza kuwa hatua hiyo,
imewaweka pabaya wapinzani waliokuwa wanapinga kila kitu.
Dk Mwakyembe alisema tatizo ni kwamba kwa hotuba hiyo, yeyote
akijaribu kuipinga, wananchi watamuona wa hovyo. Aliendelea kusema;
“Wamejaribu (upinzani) kutoka kwenye mjadala, kwa hoja tu ya TBC
(Shirika la Utangazaji Tanzania), ili wasiwepo kwenye mjadala, kwani
wakiwepo lazima wataisifia tu.”
0 comments:
Post a Comment