Thursday, January 28, 2016




Rais Magufuli wakati anaongea na wafanyabiashara Ikulu alisema alikaa na Kimei na kugundua taasisi nyingi za serikali zimehifadhi pesa nyingi sana kwenye taasisi za fedha ambazo serikali inaenda kukopa kwazo hivyo serikali kufanya biashara na fedha zake yenyewe.
Sasa serikali imeagiza serikali na taasisi zake kuondoa fedha zake katika mabenki ya biashara na kufungua akaunti benki kuu ambako itazihifadhi.

Kutokana na benki kuu kutokuwa na matawi yaliyosambaa nchi nzima, serikali imetoa ruhusa kwa taasisi hizo kuwa na akaunti kwenye benki za biashara ambapo wataweka fedha zinazotosheleza kutimiza majukumu yao ya kifedha kwa kipindi cha mwezi mmoja.

0 comments:

Post a Comment