Monday, January 25, 2016

Jana mmoja ya Viongozi wa shrikisho la Vyuo vikuu CCM Ndugu Ally S.  Hapi alitoa TAMKO Zito la kumtaka Mwanasiasa na Kada wa CCM MNEC Bernad Membe aache  kumkosoa Rais wa Jamhuri John Pombe Magufuli kuhusu kufuta safari za nje na kuhusu ukubwa wa Baraza la Mawaziri.

Hata hivyo baadae iliibuka taarifa moja kwenye Mitandao ya Kijamii kilichoonekana kuwa ni TAMKO la mwenyekiti wa Shirikisho hilo Bi Zainab Abdallah.

YAH: KUKANUSHA TAARIFA ILIYOTOLEWA KWA JINA LANGU
Nimepokea Na kuona taarifa inayozunguka Katika mitandao ya Kijamii ikionekana kuwa imetolewa Na Mimi Kama mwenyekiti wa Shirikisho. Taarifa Hiyo yenye jina langu inaeleza kuwa nimepinga Na kukanusha taarifa ya Kiongozi Mwenzangu Wa Shirikisho ambaye awali alikuwa ametoa Taarifa yenye Maudhui ya Kumjibu MNEC Benard C. Membe.

Napenda kuwataarifa Watanzania wote kuwa Mimi mwenyekiti wa Shirikisho sijatoa Taarifa yeyote Leo hii Na wala sijashiriki kikao chochote Cha Shirikisho ambacho ndio kinanipa Jambo lolote la kulitolea Taarifa.

Napenda ieleweke kwa Watanzania wenzangu wote kuwa Uongozi ni Vikao. Mimi nikiwa Kama Mwenyekiti wa Shirikisho nitatoa taarifa yeyote baada ya Kukaa Na Wajumbe wenzangu kwa mujibu wa Kanuni zetu. Hivyo wananchi Mtambue kuwa taarifa iliyotolewa kwa jina langu siijui Na siyo yangu bali ni ya kutungwa tuu Na watu ambao sielewi malengo Yao ni nini.

Mwisho napenda kuwaomba Watanzania wote tuendelee kumuunga Mkono Rais Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ili aendelee kuwaletea mabadiriko Watanzania Kama alivyoahidi.

Nawashukuru sana Na nawatakia Ujenzi Mwemba wa Taifa.
M/kiti wa Shirikisho Taifa,
Zainab Abdallah

24.Januari 2016

0 comments:

Post a Comment