Katika mchezo huo uliopigwa nchini Afrika Kusini ukiwa ni wa kwanza wa raundi ya kwanza ya michuano hiyo, Azam imejipatia ushindi wa mabao 3-0 ndani ya dakika 9.
Mchezo huo ulianza kwa kasi kwa timu zote kushambuliana huku Azam wakionekana kujiamini zaidi licha ya kuwa ugenini na kusukuma mashambulizi ya nguvu, ambapo hadi kipindi cha kwanza kinamalizika, timu zote zilikuwa hazijafungana.
Mabao ya Azam yaliyopatikana kipindi cha pili yamefungwa na Salum Abubakary Sure Boy katika dakika ya 51 kwa shuti kali nje ya eneo la 18 kufuatia kona iliyochongwa na Messi na kuokolewa vibaya na mabeki wa Wits.
Shomari Kapombe akafunga bao la pili dakika ya 56 baada ya mabeki wa Wits kufanya uzembe na mfungaji huyo akaserereka chini na kupiga shuti lililomshinda kipa wa Wits na dakika 3 baadaye nahodha John Bocco akifunga bao la tatu dakika ya 59.
Azam FC iliweza kucheza kandanda safi kwa takribani muda wote huku ikishangiliwa na watanzania takribani 200 wanaoishi nchini Afrika Kusini.
Kwa matokeo hayo, njia sasa ni nyeupe kwa Azam kusonga mbele, kwani itahitaji sare aina yoyote au isifungwe zaidi ya 3-0, katika mchezo wa marudiano utakaopigwa Chamazi jijini dare s salaam, ili isonge mbele.


0 comments:
Post a Comment