Saturday, March 19, 2016

Abiria 55 na wafanyakazi 6 mpaka sasa waliokuwa ndani ya ndege ya FlyDubai Boeing 737 -800 wamepoteza maisha baada ya ndege hiyo kupata ajali ikijaribu kutua katika hali mbaya ya hewa uwanja wa ndege wa Rostov-on-Don, Russia. Jumla ya watu ndani ya ndege walikuwa 61.


Ndege hiyo ilianguka mita mia moja kabla ya kufikia uwanja wa Rostov-on-Don.

Ndege hiyo ilikuwa imetoka Dubai flight number FZ981 na kujaribu kutua katika uwanja wa jimbo la Rostov, Rostov-on-Don.

FlyDubai hufanya safari mbili kwa wiki kati ya viwanja hivyo viwili yaani Dubai na Rostov-on-Don.

0 comments:

Post a Comment