Wednesday, March 23, 2016

Na Fatma Amir

ALIYEKUWA Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,  Said Meck Sadiki, amefunguka kwa kusema moja ya changamoto  aliyokumbana nayo wakati akiwa Dar es Salaam, ni vuguvugu la uchaguzi mkuu la mwaka 2010.

Uchaguzi huo ulihusisha wagombea wa vyama vyote wakiwemo Rais Mstaafu Dk. Jakaya Kikwete wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Dk. Wilbroad Slaa aliyegombea kwa tiketi ya chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
Sadiki ambaye sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam katika sherehe ya kuagwa iliyohusisha viongozi wa dini wa kiislam na Kikristo.
Aidha, aliwaomba viongozi wa dini wamuunge mkono Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, katika kampeni ya ‘kusafisha jiji ondoa uchafu’.

“Wananchi wa Dar es Salaam ndio wamenifikisha hapa nilipo,  hadi  Rais Magufuli alipoamua kunipeleka  Mkoa wa Kilimanjaro kwenda kuendeleza mazuri niliyoyafanya hapa,” alisema
Aidha, aliwaomba viongozi wa dini kuendelea kumwombea ili akafanye kazi kama alivyokuwa akiifanya alipokuwa Dar es Salaam.

“Nikuombea Makondaufanye kazi  pamoja na kamati ya viongozi wa dini uwashirikishe changamoto utakazokumbana nazo ili wakusaidie katika kukuombea,” alisema.
Makonda aliendelea kusisitiza kuhusu mpango aliopanga kuanza nao wa kuondoa gereji zilizopo mitaani, baana yadi za magari zihamie maeneo maalum lengo likiwa ni kuifanya Dar es Salaam kuwa safi.

 “Uchafu unaanzia moyoni mwako, nawaomba wananchi kila mmoja asafishe maeneo yao,” alisema.

Aidha, amewataka viongozi wa Serikali ya Mtaa wampatie idadi ya wananchi wanaoishi eneo yao ili ulinzi uweze kuimarishwa.
“Nashukuru Rais John Magufuli kwa kunichagua kufanya nae kazi, namshukuru baba yangu Meck Sadiki  leo ni siku iliyofungua kurasa mpya ambayo sikuwahi kuusoma,”alisema

Kwa upande wake aliyekuwa  mgeni rasmi Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki Abdula Ally Hasani Mwinyi alisema kwa upande wake hana tatizo na uongozi wa Paul Mkaonda yeye ni kiongozi bora.

“Matatizo yakukosa amani yana vyanzo vingi ikiwemo dini, wananchi kukosa kipato, uhaba wa risilimali na hayo ndio yanayodumaza maendeleo ya taifa.”alisema Mwinyi
Mwinyi alimtaka Makonda kuwa msikivu kwa viongozi wa dini na viongozi wengine ili kuwa kiongozi bora.

Mwisho

0 comments:

Post a Comment